Thursday, October 20, 2011

Oct NGORONGORO HEROES YAPANGWA NA SOUTH AFRICA COSAFA CUP


Timu ya taifa chini ya miaka 20 Ngorongoro Heroes ipangwa kundi C pamoja na South Africa katika michuano ya vijana ya COSAFA itakayofanyika nchini Botswana.

Ngorongoro heroes itashiriki kama timu mualikwa katika mashindano hayo yanayohusisha timu za Taifa za vijana chini ya miaka 20 kwa mataifa ya kusini mwaafrica.

Ngorongoro wamepangwa kundi C pamoja na South Africa, Zambia, na Mauritius, wakati kundi A lina timu za Botswana, Comores, Swaziland na Mozambique.

Kundi B lina timu toka Seychelles, Malawi, Lesotho na Zambia na Kundi D lina timu za Angola, Madagascar, Namibia na Zimbabwe.

Mashindano hayo yanatarajiwa kuanza december 01 mwaka huu kwa mchezo kati ya Botswana na Comores, wakati Swaziland ikiwakabili Mozambique siku hiyo ya ufunguzi.

Ngorongoro watafungua kwa kucheza na Zambia december 2 wakati Angola wakicheza na Madagascar, Namibia na Zimbabwe, South Africa na Mauritius, Seychelles na Malawi siku hiyo.

No comments:

Post a Comment