Thursday, March 7, 2013

MAAFANDE WAHUSISHWA NA TUKIO LA UTEKAJI WA MWENYEKITI WA JUKWAA LA WAHARIRI, ABSALOM KIBANDA

 HII  NI  KAULI  YA  ABSALOM  KIBANDA  BAADA  YA  KUTEKWA...............
"Baada ya kutoka kwenye gari, nahisi nilikanyaga sehemu mbaya, nikateleza na kuanguka wakanifuata...niliona kama watu watatu hivi wakaanza kunishambulia. Sikuwa nafahamu kilichojiri, lakini nilisikia mwingine akimwambia mwenzake afande 'mshuti... mshuti' huyo alipoelekeza mtutu na kujaribu 'kushuti' (kupiga risasi) ilikuwa kama vile imegoma.

“Nikiwa bado niko chini, wakanipiga kwa kitu cha ncha kali kwenye jicho la kushoto, wakaning’oa meno na kucha katika vidole vya mkono wa kulia, walinipiga sana na nilipata maumivu makali. Baada ya kunipiga na kunijeruhi waliniburuza hadi bembeni ya nyumba yangu na kunitupa na wakaondoka, baadaye majirani na wasamaria wema walikuja kuniokoa..."

MASHABIKI WAIKATAA VIDEO YA OMMY DOMPOZ WASEMA KASHUKA KIWANGO

Siku chache baada ya kuachia video yake iliyokuwa inasubiriwa sana na mashabiki wa bongo fleva, matokeo yake yamekuwa sio mazuri kwa Ommy Dimpoz na video ya wimbo wake wa me and you, aliyoshoot na kampuni kutoka Kenya inayoitwa Ogopa, huku akiwa ameishoot katika maeneo ya huko huko kenya. haya ni baadhi ya maoni juu ya video ya wimbo huo